MPOLI PICTURES

I am a Writer

MPOLI PICTURES

We are a full-service wedding cinematography and photography company. We create cinematic and documentary style wedding films. Our shooting style is journalistic, inconspicuous and centered on documenting each important moment as it happens. We dedicate our work to creativity, superior quality, exceptional quality and honest value in photography. Choose us to create your memory.

  • Morogoro, TANZANIA
  • +255714845658,
  • mpolipictures@gmail.com
  • www.mpolipictures.net
Me

My Professional Skills

We are a full-service wedding cinematography and photography company. We create cinematic and documentary style wedding films.

Camera Opparating 90%
Camera Setting 70%
Video Shooting 95%
Graphics 90%
Showing posts with label News. Show all posts
Showing posts with label News. Show all posts
  • Wagombea wa Republican washindania Nevada

    Wagombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani wanakabiliana kwenye uchaguzi wa mchujo katika jimbo la Nevada katika kinyang’anyiro cha nne cha kuamua mgombea wa chama hicho.

    Mfanyabiashara Donald Trump, ambaye amekuwa akiongoza kwenye kura za maoni kitaifa, anaongoza pia kwenye kura za maoni jimbo hilo, na anatarajia kupata ushindi wa tatu mtawalia baada ya kushinda New Hampshire na South Carolina.

    Nevada, ambalo ni jimbo lisilo na mbabe na lenye watu wengi wa asili ya Amerika Kusini, ni muhimu sana katika uchaguzi.

    Upigaji kura kwa sasa unaendelea na kuna foleni ndefu vituoni.

    Kura ya maoni ya karibuni CNN/ORC imeonesha Trump ana uungwaji mkono 45% akifuatwa na Seneta Marco Rubio 19% naye Seneta Ted Cruz akiwa na 17%.

    Ingawa Nevada ina wajumbe wachache, inatarajiwa kuwa mtihani kwa Trump kutokana na matamshi yake dhidi ya wahamiaji ikizingatiwa kwamba ina watu wengi wa asili ya Amerika Kusini.

    Hillary Clinton alishinda kwenye jimbo hilo katika chama cha Democratic Jumamosi.

    Alimshinda mpinzani wake Bernie Sanders kwa kumpita kwa asilimia tano na wagombea hao wawili sasa wanaangazia jimbo la South Carolina lenye watu wengi weusi.

    Uchaguzi wa mchujo wa chama cha Republican katika jimbo la South Carolina utafanyika Jumamosi.

    Uchaguzi wa mchujo hutumiwa kuchagua wagombea wa vyama viwili vikuu kwenye uchaguzi mkuu wa urais ambao utafanyika mwezi Novemba.

    Chanzo; BBC
  • Ezekiel Maige Atajwa Ufisadi Ngorongoro

     Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii katika serikali ya awamu ya nne, Ezekiel Maige, jana alitajwa katika kesi inayomkabili aliyekuwa Mhifadhi Mkuu wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, Bernard Murunya  ambaye ameshitakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi.
    Katika kesi hiyo, Maige anadaiwa kulipiwa nauli ya safari ya nje na mamlaka hiyo kwa idhini ya Murunya, ambaye sasa ni Mbunge wa Afrika Mashariki.
    Shahidi wa kwanza katika kesi hiyo, Sezari Semfukwe, alidai kuwa Murunya na aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa Mamlaka hiyo, Shad Kiambile, waliidhinisha malipo ya dola 66,890. Alidai kuwa fedha hizo zilikuwa kwa ajili ya safari ya Maige na msaidizi wake aliyetajwa kwa jina la E. Muyungi na Murunya mwenyewe.
    Semfukwe, ambaye ni Kaimu Mhasibu Mkuu wa mamlaka hiyo, alidai kuwa Murunya na Kiambile, ndio walioidhinisha madokezo kwa ajili ya malipo hayo.
    Akiongozwa na Wakili wa Serikali Hamidu Sembano, akisaidiana na Rehema Mteta, mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Arusha, Patricia Kisinda, Semfukwe alidai kuwa utaratibu wa maombi ya safari, unatokana na maelekezo ya mkuu wa idara na kujaza fomu inayoonyesha anakwenda wapi na kwa muda gani.

    Sambamba na hilo, alidai kuwa aina zingine za safari zinahusisha watu wa nje ambao, si waajiriwa wa NCAA kwa dokezo la mkuu wa idara au shirika.
    Alidai kuwa alitoa hundi ya malipo namba 309/0238 ya Septemba 9/2011, ambayo ilikuwa na dokezo la safari kutoka kwa Murunya kwenda kwa Mkuu wa Kitengo cha Fedha. Pia  alitoa hundi ya malipo nyingine iliyokuwa ikionyesha imelipwa dola zaMarekani  66,890 kwa kampuni ya Wakala wa Usafirishaji ya Cosmas.

    Aliendelea kudai kuwa hundi za malipo namba 310/0379 ya Oktoba 29, 2011 na ankara namba 5609 ya Septemba 7,  2011 zililipwa kwa Antelope Tours & Traveling kwa ajili ya tiketi za Murunya, Muyungi na Maige kwa malipo ya dola za Marekani 66,890 (zaidi ya Sh. milioni 133).
    Shahidi hiyo alidai kuwa kumbukumbu ya kitabu cha malipo ya hundi inaonyesha hundi namba 002758 na 002755 za Septemba 9,  2011 zililipwa kwa kampuni ya Cosmas Travelling Agent na zilitiwa saini na Kiambile na Murunya.

    Hata hivyo, wakati shahidi huyo akitoa vielelezo hivyo mahakamani hapo ili vitumike kama ushahidi, malumbano ya kisheria yaliibuka baina ya mawakili wa pande zote.

    Malumbano hayo yaliibuka baada ya upande wa washtakiwa, ukiongozwa na wakili Amani Mirambo, kutaka kujua ni vielelezo vingapi au vya aina gani ambavyo upande wa mashtaka unavileta.

    Hatua hiyo ilisababisha malumbano ya kisheria hivyo kumfanya hakimu kuahirisha kesi kwa dakika 10. Baada ya muda huo, alirejea mahakamani baada ya dakika hizo na kuwahoji.

    Baada ya kuhoji pande zote mbili, kutokana na malumbano ya kisheria, Hakimu alikatizwa na Wakili wa Serikali Hamidu Simbano, aliyemwomba  kuahirisha kesi hiyo na kutaja tarehe nyingine ya  washtakiwa kusomewa maelezo yao ya awali.

    Awali, Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Rehema Mteta, aliwasomea maelezo ya awali juu ya tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka yaliyosababisha mamlaka hiyo kupoteza dola 66,890 (Sh. 133,780,000).

    Mteta aliwataja washitakiwa, mbali na Murunya na Kiambile, kuwa ni Meneja Utalii wa mamlaka hiyo, Veronica Funguo na Salha Issa ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Cosmas Travelling Agent.
    Chanzo; MPEKUZI
  • Jamhuri ya Afrika ya Kati wapiga kura

    Wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati wamepiga kura kumchagua rais mpya katika uchaguzi unaorudiwa baina ya waliokuwa mawaziri wakuu, Faustin Touadera na Anicet Dologuele.

    Pia watachagua wabunge baada ya uchaguzi uliofanywa mwezi Disemba mwaka jana kubatilishwa kutokana na kasoro zilizojitokeza.

    Mwandishi wa BBC Abdourahmane Dia kutoka Bangui anasema mara hii, wananchi hawakuwa na hamasa kubwa ya kupiga kura, ingawa maafisa wa tume ya uchaguzi wanasema upigaji kura umefanyika vizuri.

    Wapiga kura wanachagua rais wao na wabunge wao katika uchaguzi ambao unatarajiwa kumaliza mapigano ya zaidi miaka mitatu baina ya jamii za nchi hiyo.

    Hakuna matukio makubwa yaliyoshuhudiwa, lakini vituo vya kupigia kura vilionekana vikiwa na wapiga kura wachache, ikilinganishwa na uchaguzi uliofanyika mara ya kwanza, hayo ni kwa mujibu wa mwandishi wa BBC ambae yuko katika mji mkuu wa Bangui.

    Tatizo la mipango na ukosefu wa baadhi ya vifaa umetawala uchaguzi huo kama walivyoeleza baadhi ya wapiga kura.

    "nimeshindwa kupiga kura kwa sababu jina langu halipo katika daftari la kupiga kura. Na mara ya mwisho niliweza kupiga kura, lakini leo wamekataa. Inaumiza, ni uonevu kwa sababu mimi ni raia pia."

    "nimeshindwa kuona jina langu na mara ya mwisho nimepiga kura hapa. Nimeangalia kila sehemu lakini sijaona jina langu. Sijui nitafanya nini sasa."

    Hata hivyo, maafisa wa tume ya uchaguzi wamesema kwamba hatua mpya zimechukuliwa ili kuepusha mapungufu hayo.

    Marudio ya uchaguzi huo yanafanyika mwezi mmoja na nusu baada ya mchuano wa mara ya kwanza ambapo wagombea thelathini waliingia kwenye kinyang'anyiro cha urais.

    Wagombea wote wawili Anicet Dologuele, ambae amebobea katika maswala ya benk na Faustin Touadera, ambae ni mhadhiri wa chuo kikuu, wote wanasimamia umoja wa kitaifa, usalama, na uchumi.

    Hata hivyo, atakaeibuka kidedea, atatakiwa haraka sana, atatue tatizo la makundi yenye kumiliki silaha ambayo bado yana nguvu katika maeneo mbali mbali ya nchi licha ya kuwepo kwa vikosi vya kulinda amani elfu kumi na moja vya Umoja wa Mataifa.
  • ACT-Wazalendo Waungana na CUF kupinga Uchaguzi wa Marudio Zanzibar........Wamtaka Rais Magufuli Afute Posho za Makalio Na Matumizi Ya Magari Ya Anasa

     Maazimio Ya Kamati Kuu Ya ACT-Wazalendo Kufuatia Kikao Chake Kilichofanyika Jumamosi 13 Februari 2016 Katika Hoteli Ya Kagame Jijini Dar Es Salaam

    Kamati Kuu ya Chama cha Wazalendo (ACT-Wazalendo) ilifanya kikao chake cha kawaida siku ya Jumamosi tarehe 13 Februari 2016 katika Ukumbi wa Hoteli ya Kagame Jijini Dar es Salaam.

    Pamoja na mambo mengine, Kamati Kuu ilijadili, kutolea maoni na kuazimia mambo yafuatayo yanayohusu chama na Taifa kwa ujumla.

    1. Kamati Kuu ilijadili na kuzingatia hali ya kisiasa nchini na kutolea maoni mambo yafuatayo:

    a. Kamati Kuu iliwapongeza wananchi na Tume ya Taifa Uchaguzi (NEC) kwa kufanikisha uchaguzi mkuu kwa amani kwa upande wa Jamhuri Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Kamati Kuu inalaani kitendo cha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi wa Zanzibar za kuvuruga zoezi la kukamilisha kujumlisha matokeo ya kura zilizopigwa katika uchaguzi huo.

    b. Kamati Kuu ilipokea na kujadili utendaji wa serikali ya awamu ya tano ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais John Pombe Joseph Magufuli na kuzingatia yafuatayo:

    i. Kamati Kuu imetambua jitihada za serikali ya Dk Magufuli katika kupambana na rushwa na ufisadi nchini kupitia dhana ya kile anachokiita ‘kutumbua majipu’. Hata hivyo, Kamati Kuu imezingatia kuwa bado hali ya maisha ya wananchi imeendelea kuwa ngumu kama inavyothibitishwa na kuendelea kupanda kwa bei ya bidhaa muhimu kwa maisha ya binadamu kama vile sukari, mchele, na mafuta ya kula. Aidha, pamoja na bei ya mafuta kuendelea kushuka kwa kasi katika soko la mafuta duniani, bei ya mafuta hapa nchini imeshuka kwa kiwango kidogo kisicholingana na kiwango cha kushuka katika soko la dunia.

    ii. Pamoja na kwamba chama chetu kinaunga mkono juhudi za kuwachukukia hatua za kinidhamu watumishi wa umma wenye tuhuma za rushwa na ubadhirifu wa mali za umma, tunasisitiza kwamba juhudi hizo lazima zifanywe kwa kuzingatia misingi ya utawala wa sheria, utawala bora na utu.

    Aidha, serikali ya Rais Magufuli haijajikita katika kuleta mabadiliko ya kimfumo, ikiwemo: kubadili mikataba ya kinyonyaji ya raslimali kama vile madini na mafuta; kufuta posho za makalio katika mfumo wa utumishi wa umma ikiwemo Bunge; kuachana na matumizi ya magari ya anasa (mashangingi); tunaendelea kuagizi sukari nje; hakuna mpango wa kuifanyia mabadiliko TAKUKURU; na serikali haielekei kama itashughulikia suala la Katiba Mpya ambayo ndiyo ajenda kubwa kwa miaka mingi sasa.

    2. Kamati Kuu imepokea na kujadili hali ya kisiasa katika visiwa vya Zanzibar na kuzingatia na kuazimia yafuatayo:

    a. Kamati Kuu imeendelea kusisitiza kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar, Ndugu Jecha Salumu Jecha, hakuwa na uhalali wa kisiasa, kikatiba na kisheria kufuta zoezi lililokuwa linaendelea la kuhesabu kura mnamo tarehe 28 Oktoba 2015.

    Dalili zote za kisiasa zinaonyesha kwamba Ndugu Jecha alichukua hatua alizochukua kwa shinikizo na/au mapenzi ya kisiasa kwa lengo la kuzuia ushindi wa chama kimojawapo ulioelekea kuwa dhahiri.

    Kamati Kuu imezingatia pia kuwa, mbali na Chama cha Mapinduzi, waangalizi wote wa uchaguzi wa ndani na nje, pamoja na Jumuiya ya Kimataifa, ikiwemo Jumuiya ya Afrika Mashariki, wametamka bayana kwamba uchaguzi wa Zanzibar ulifanyika katika mazingira ya haki, huru na demokrasia na matokeo ya uchaguzi huo yalizingatia utashi na matakwa ya wapiga kura wa Zanzibar.

    Kwa kuzingatia haya, Kamati Kuu imeazimia yafuatayo:

    i. Kupinga marudio ya uchaguzi uliopangwa kufanyika tarehe 20 Machi 2016 na kwamba Chama chetu cha ACT-Wazalendo hakitashiriki katika uchaguzi huo

    ii. Kutoa wito maalumu kwa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania kuchukua hatua stahiki kwa mamlaka aliyepewa kikatiba kuhakikisha kwamba Umoja na Amani ya Taifa inaendelea kuimarika nchini kwa kuzingatia misingi ya demokrasia, utawala wa sheria na utawala bora.

    iii. Kamati kuu ya ACT-Wazalendo,inataka madiwani na wawakilishi walioshinda na kutangazwa rasmi na ZEC katika uchaguzi uliofanyika Oktoba 25/2015 watambuliwe na waanze kuwatumikia wananchi.

    Kwa sababu wawakilishi na madiwani waliotangazwa na ZEC ni halali kwa mujibu wa katiba, sheria na kanuni za Uchaguzi wa Zanzibar

    iv. Kamati Kuu inaamini kwamba suluhu ya mkwamo wa kisiasa Zanzibar ni kufanya mazungumzo yatakayojumuisha wadau wote muhimu katika mchakato wa uchaguzi wa Zanzibar. Hatuamini kwamba mkwamo huu utatuliwa kwa vitisho vya kidola.

    3. Kamati Kuu imepokea, kujadili na kupitisha taarifa ya uchaguzi wa chama na kuzingatia yafuatayo:

    a. Kamati Kuu imewapongeza na kuwashukuru wananchi waliojitokeza kupiga kura na kukiunga mkono chama na hata kufanikiwa kumpata mbunge mmoja, madiwani 41 katika mikoa mbalimbali, na kuongoza Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji

    b. Kamati Kuu imepitisha taarifa ya mapato na matumizi katika uchaguzi mkuu ambapo chama kilipokea na kutumia shilingi 656,625,000/=.Taarifa hii inawekwa wazi kwa umma kama tulivyoahidi kwa kuzingatia tunu yetu ya uwazi

    c. Kamati Kuu imevipongeza vyombo vya habari kwa kazi kubwa waliofanya katika kuwaelimisha wananchi kuhusu uchaguzi mkuu na kwa kufanya kazi kwa weledi na bila ubaguzi

    4. Kamati Kuu imejadili na kupitisha Mkakati wa Chama kwa kipindi cha miaka mitano 2016-2020.

    Mkakati huu unalenga kukiimarisha chama katika maeneo matano yafuatayo:

    i) Kuimarisha safu ya uongozi na watendaji katika ngazi zote
    ii) Kuimarisha mfumo wa mawasiliano ya ndani na kwa umma
    iii) Kuibua na kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo ya wananchi kwa kuwashirikishi wananchi
    iv) Kuimarisha mahusiano na vyombo vya habari
    v) Kujiandaa kikamilifu na kimkakati kwa chaguzi za serikali za mitaa wa mwaka 2019 na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, na chaguzi ndogo zitakazojitokeza.

    5. Ili kutekeleza kikamilifu Mkakati wa Chama, pamoja na hatua zingine, Kamati Kuu imeziunda upya Kamati za chama makao makuu kama ifuatavyo:

    i) Kamati ya Fedha na Miradi ya Kujetegemea
    ii) Kamati ya Utafiti, Sera na Mipango
    iii) Kamati ya Uadilifu, Ulinzi na Usalama wa Chama
    iv) Kamati ya Katiba, Sheria na Mambo ya Nje
    v) Kamati ya Itikadi, Mawasiliano na Uenezi
    vi) Kamati ya Maendeleo ya Jamii
    vii) Kamati ya Mafunzo na Chaguzi
    viii) Kamati ya Wabunge na Uendeshaji wa Serikali za Mitaa

    Kamati kuu imeiagiza sekretariet ya chama kuanza utekelezaji wa mpango mkakati, ili kukiandaa chama kwa Uchaguzi ujao na uchaguzi mbali mbali

    Pia kamati kuu inawahimiza wanachama waendelee na juhudi za ujenzi wa Chama na kutunza amani ya nchi.

    Zitto Ruyagwa Kabwe
    Kiongozi wa Chama
    14/02/2016
  • CUF: Maalim Seif Sharif Hamad Akishinda Uchaguzi wa Marudio Zanzibar Hatakubaliana Na Matokeo

     Chama cha Wananchi (CUF) kimesema ikitokea Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Maalim Seif Sharrif Hamad ameshinda kwa kupigiwa kura na akaibuka mshindi wa kiti cha urais katika uchaguzi wa marudio utakaofanyika Machi 20, hatakwenda kuapishwa.

    Kimesema kuna uwezekano mkubwa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), ikaweka jina la Maalim, wawakilishi na madiwani katika karatasi za kupigia kura na kusisitiza, ikitokea hivyo na wagombea hao wakapigiwa kura, wote hawataenda kuapa.

    “Kama wagombea wetu wakichaguliwa na ZEC ikawatangaza washindi itakuwa ni kazi bure. Pia, CUF hatutakwenda mahakamani kufungua kesi ya kikatiba kupinga hatua ya mwenyekiti wa ZEC kufuta matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25,” Kaimu Katibu Mkuu wa CUF, Nassor Ahmed Mazrui aliwaambia waandishi wa habari jana.

    Oktoba 28, mwaka jana mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha alifuta matokeo ya uchaguzi wa rais, wawakili shi na madiwani kwa maelezo kuwa sheria na kanuni zilikiukwa na baadaye kutangaza Machi 20 kuwa siku ya kupiga kura upya.

    Mazrui alisema licha ya CUF kuiandikia barua ZEC, ikitaka wagombea wake wote kuondolewa katika orodha ya karatasi ya kupigia kura, kuna uwezekano mkubwa wa majina hayo kutoondolewa.

    “... Sisi tumeshaipelekea ZEC barua 54 za wawakilishi na madiwani walioshindwa au kushinda katika uchaguzi wa Oktoba 25 na kuwaeleza kuwa wawaondoe katika karatasi za uchaguzi wa marudio.

    "Hata kama wananchi watamchagua Maalim Seif kwa asilimia 90 hawezi kwenda kuapishwa. Kufanya hivyo ni sawa na kukataa kula nyama ya nguruwe lakini mchuzi wa nyama hiyo unaunywa.”

    Mazrui ambaye alitangazwa mshindi wa uwakilishi wa jimbo la Mtopepo, kabla ya kufutwa kwa matokeo hayo alisema, “Hatuna shida na uchaguzi wao, tumekosa nini mpaka tuwe na shida nao?”

    Alisema CCM inadhani kwamba CUF itajitosa kushiriki uchaguzi huo wa marudio katika dakika za mwisho; “wanachotakiwa kujua ni kwamba hatuingii katika uchaguzi wao wawe na amani yote.”

    Akizungumzia kauli ya Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu kwamba CUF walipaswa kupinga kufutwa kwa matokeo ya uchaguzi, siku 14 baada ya kutangazwa, Mazrui alisema kauli hiyo imedhihirisha kuwa hata wakienda mahakamani hakuna haki itakayotendeka.

    “Ameshatoa hukumu kabla hata kesi haijafunguliwa. Muda wa siku 14 aliousema unahusu ukomo wa kupeleka kesi ya uchaguzi Mahakama Kuu. Kesi ya uchaguzi msingi wake mkubwa ni uamuzi wa msimamizi wa uchaguzi ambao CUF na wajumbe wateule hatuna tatizo nao,” alisema.

    “Hakuna anayetaka atangazwe mshindi kati ya wagombea wote wa CUF kwa kuwa walitangazwa kihalali na wasimamizi wa uchaguzi na kupewa vyeti.

    "Aliyehujumu uchaguzi si ZEC ni Jecha. Sisi kesi tunayoweza kufungua ni ya kikatiba si kupinga matokeo na kesi ya kikatiba haina muda wa kufungua kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar.”

    Alisema kutokana na kauli ya Makungu, CUF imewashauri wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliokuwa na nia ya kupeleka shauri mahakamani kuachana na wazo hilo kwa maelezo kuwa Jaji Makungu ameshaandaa hukumu na kuisoma hadharani.

    Chanzo; Mpekuzi blog
  • Mwanamke Aliyemkaba Jambazi Na Kumpora Bunduki Aina Ya SMG Azawadiwa Laki 5 Na Jeshi La Polisi

    Mwanamke aliyepambana na jambazi na kufanikiwa kumnyang’anya bunduki aina ya SMG, Sophia Manguye (46), amepewa zawadi ya Sh 500,000 na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Gemini Mushy. 

    Mwanamke huyo ambaye aliomba Serikali kumpa silaha ili kujilinda, alisema kuwa hajaridhika na zawadi hiyo kwa kuwa kama asingemmudu jambazi huyo watu wengi wangepoteza maisha.

    Hata hivyo, Mushy alimwomba Manguye kupokea kiasi hicho japokuwa ni kidogo kwa kuwa ni zawadi kutoka ofisi yake.

    Tukio hilo lilitokea Februari 9, saa 2.42 usiku, baada ya watu watatu kufika dukani kwake, mmoja wao akiwa na bunduki kisha kumwamuru atoe fedha alizokuwa nazo.

    Manguye alisema alichukua Sh80,000 alizokuwa nazo na kumkabidhi jambazi huyo, lakini hakuridhika na kumlazimisha aongeze kiasi kingine.

    “Nilipandwa hasira nikanyanyuka wakati jambazi anainama kuangalia kwenye kiboksi cha fedha, nikamkamata kifuani na kung’ang’ania mkanda wa bunduki, akaanza kunivuta kwenda nje, nami nikamvutia ndani, lakini alifanikiwa kunitoa nje akaniangusha chini, lakini sikuachia mkanda wa bunduki,” alisema Manguye na kuongeza:

    “Aliposikia wananchi wameanza kupiga yowe akaniachia na kutoa mkanda wa silaha begani, akakimbia na kuniachia bunduki. Wakati huo huo jambazi mwingine alikuwa amekamatwa kwenye duka la Zaituni Magasi, wananchi walipofika wakaanza kumshambulia, wakati huo taarifa ilikuwa tayari imetolewa Kituo cha Polisi Sirari, wakafika kumchukua,” alisema.

    Hii ni mara ya pili kwa Manguya kuvamiwa na majambazi wenye silaha, ambapo mwaka 2014 alivamiwa dukani kwake na majambazi waliokuwa na bunduki, lakini alifanikiwa kumpiga kwa kigoda aliyekuwa na bunduki na alianguka chini.

    Magasi alisema wakati wa tukio hilo, alikuwa amevamiwa na majambazi waliokuwa na bunduki, mapanga na nondo.

    “Wakati anatoka mvunguni mdogo wangu alimkamata kwa nyuma na kummudu huku akipiga kelele, watu wakafika wakaanza kumpiga hadi akazimia, polisi walipofika wakamwokoa kwani kidogo wamuue,”alisema. 
  • CUF Yasema Ipo Tayari Kwa Mazungumzo ila Sio Kurudia Uchaguzi

    ikiwa  zimebaki siku chache kabla ya kurudiwa kwa uchaguzi Zanzibar, Makamu wa Kwanza wa Rais Maalim Seif Sharrif Hamad amehoji sababu za chama tawala, CCM kuhofia CUF kuongoza visiwa hivyo.

    Maalim Seif, ambaye aligombea urais wa Zanzibar katika uchaguzi wa Oktoba 25 ambao matokeo yake yalifutwa, pia amesema endapo CCM itasitisha uchaguzi huo uliopangwa kufanyika siku 36 zijazo, CUF watakuwa tayari kufanya mazungumzo lakini si kwa wakati huu ambao maandalizi ya kupiga kura yanaendelea.

    Akizungumza na waandishi wa habari jana, katibu huyo mkuu wa CUF aliitoa hofu CCM kuwa chama chake hakina ajenda ya kulipiza kisasi.

    Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar, wawakilishi na madiwani yalifutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (ZEC), Jecha Salum Jecha siku ambayo chombo hicho kilitakiwa kumtangaza mshindi, na mwezi uliopita alitangaza Machi 20 kuwa siku ya uchaguzi wa marudio visiwani humo.

    Wakati CUF ikipinga vikali kufutwa matokeo na kutangaza tarehe mpya, Serikali imesema kuna nafasi ya kufanya mazungumzo kabla ya uchaguzi wa marudio kwa kuwa kuna muda  mrefu wa kufanya hivyo.

    Jecha alitangaza uamuzi huo wakati tayari matokeo ya urais ya majimbo 31 yalishatangazwa, na ya majimbo tisa yaliyosalia yalishahakikiwa, huku washindi wa viti vya uwakilishi na udiwani wakiwa wametangazwa na kupewa vyeti vya ushindi.

    “Sijui kwa nini CCM wanaogopa sisi tukiongoza?” alihoji Maalim Seif kwenye mkutano huo na waandishi akiwa pamoja na aliyekuwa mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa.

    “Wana wasiwasi gani, kwamba CUF ikiongoza kutatokea nini? Sisi hatuna ajenda ya kulipiza kisasi,” alisema.

    Katika mkutano huo, Maalim Seif mbaye pia ni katibu mkuu wa chama hicho alisema kama CCM ina wasiwasi na idadi ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), haina budi kuondoa shaka kwa kuwa idadi kwa pande zote inakaribiana.

    “Hawa wanahisi hawatapata uwakilishi mkubwa, lakini mbona miaka yote tunakuwa na idadi isiyopishana ya wawakilishi?” alihoji.

    Kuna Vitisho  Zanzibar
    Katika mkutano huo, Maalim Seif alisema kumekuwapo vitendo vya wananchi kupigwa na vikundi vya watu wasiojulikana.

    Alidai wafanyakazi wa Serikali na taasisi zake wameamrishwa kupeleka vitambulisho vyao vya kazi na vya kura serikalini ili vikahakikiwe.

    “Hii si mara ya kwanza wafanyakazi wa Serikali kutakiwa kupeleka vitambulisho, sisi tunajua kuwa wanataka wawatishe kuwa watajua nani kapiga kura na nani hajapiga,” alisema na kusisitiza:

    “Hii ni kama kitisho cha kuwalazimisha wakapige kura, zaidi hasa hizo ni dhuluma ambazo wananchi wanafanyiwa.”

    Kadhalika Maalim Seif alizungumzia uwapo wa watu wanaovaa soksi usoni na kuwashambulia raia, akisema Serikali haijachukua hatua stahiki kudhibiti hali hiyo.

    Alisema watu hao ambao wamepachikwa jina la mazombi, wamevamia maeneo kadhaa kama Baraza la CUF, Jang’ombe na yaleambayo yana wafuasi wa chama hicho kikuu cha upinzani visiwani humo.

    “Wanawapiga watu, wanawajeruhi na wanaiba mali, lakini inashangaza sana mambo haya na si Serikali wala polisi iliyochukua hatua,” alisema.

    Maalim Seif alisema amezungumza na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein kuhusu matukio hayo ya uharamia wanaofanyiwa wananchi, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa.

    Alisema CCM wanatafuta sababu ili machafuko zaidi yatokee visiwani humo wapate kisingizio.

    Aliwataka wafuasi wa CUF kuvumilia hali hiyo ili nchi isiingie kwenye machafuko kama yaliyotokea mwaka 2000, wakati watu zaidi ya 20 waliuawa na wengine kukimbilia Shimoni, Mombasa nchini Kenya ambako waliishi kama wakimbizi.

     Lowassa Azungumza
    Kwa upande wake, Lowassa aliwataka viongozi wa ngazi za juu wachukue   hatua kumaliza mgogoro wa Zanzibar.

    “Hili tulichukulie kwa umakini sana. Viongozi wafanye vikao vya maridhiano, tunaipenda sana amani tuliyonayo,” alisema.

    Lowassa alisema anashangazwa na jinsi CCM wanavyoshindwa kuheshimu makubaliano ya SUK na kukataa kukubali matokeo.

    ZEC  yagoma  kuondoa  picha  ya  Maalim
    Wakati huohuo, habari zinaarifu kuwa Tume  ya  Uchaguzi  Zanzibar( ZEC)  imegoma  kuondoa  picha  za  wagombea  Urais,Udiwani  na Uwakilishi  kutoka  vyama  vilivyotangaza  kutoshiriki  uchaguzi  wa  marudio,ikiwemo  jina  na  picha  Maalim Seif Sharif Hamad.

    Hilo  lilifahamika  jana mjini Unguja  baada  ya  kigogo  mmoja  wa  ZEC ambaye  hakuwa  tayari  kutaja  jina  kusema  kuwa  sheria  hazimruhusu  mgombea  yeyote  kujitoa  mwenyewe  kwa  utashi  wake  binafsi.

    Kiongozi  huyo  alisema  kwa  mujibu  wa  kifungu  cha  36  cha  sheria  ya  uchaguzi  namba  11  ya  mwaka  1984,mgombea  hawezi  kujiondoa  kwa  utashi  wake  baada  ya  Tume  kukamilisha  kazi    ya  uteuzi  ambayo  ilifanyika  kabla  ya  Oktoba  25  mwaka  jana.

    "Ieleweke  kwamba mgombea  urais  anaweza  kujiondoa  katika  kinyang'anyiro  kwa  kuwasilisha  taarifa  za  maandishi  yeye  mwenyewe  ofisi  za  ZEC  kabla  ya  saa 10  jioni  ya  siku  ya  uteuzi." Alisema  ofisa  huyo  akinukuu  kifungu  cha  katiba.

    Alisema  uteuzi  wa  mgombea  mwingine  unaweza  kufanyika  ndani  ya  siku 21  kama  mgombea  hatafariki dunia,lakini  hakuna  ruhusa  ya  kujitoa  kabla  ya  kukamilika  kwa  uchaguzi.

    Alisema  ZEC  tayari  imeviandikia  vyama  kuvitaka  vithibitishe  iwapo  wagombea  wao  wangali  hai  au  kuna  waliofariki dunia, na si kutaka  kufahamu  kama  watashiriki  uchaguzi  wa  marudio  au  la.

    Mkurugenzi  wa  Mipango  na  Uchaguzi CUF  anena
    Mkurugenzi  wa  Mipango  na  Uchaguzi  wa  CUF, Omar Ali Shehe  amesema  ZEC  inasuka  mkakati  wa  siri  wa  kutaka  kuzitumia  picha  na  taarifa  za  wagombea wao  kwa  lengo  la  kuidanganya  dunia  na  jumuiya  za  kimataifa  kwamba  CUF  walishiriki  uchaguzi  huo.

    Shehe  amesema  CUF  kilitangaza  mapema  kabisa  kutoshiriki  uchaguzi  wa  marudio,hivyo  dunia  nzima  inaelewa  kabisa  kwamba  CUF  haishiriki  uchaguzi  huo  na  kitendo  cha  kuendelea  kuchapisha  picha  na  taarifa  za  wagombea  wao  katika  karatasi  za  wapiga  kura  si  sahihi.

    Chanzo; Mpekuzi blog
  • Rwanda kuwahamisha wakimbizi wa Burundi

    Serikali ya Rwanda imetangaza kwamba itawahamisha mara moja wakimbizi wa Burundi hadi mataifa mengine.

    Waziri wa maswala ya kigeni Luoise Mushikwabo amesema kuwa ukosefu wa maelewano haukubaliki ,baada ya mjumbe mmoja wa Marekani kuzungumzia kuhusu ripoti kwamba Rwanda imekuwa ikiwapa mafunzo wakimbizi wa Burundi ili kukabiliana na serikali ya Burundi.

    Rwanda kwa sasa inawahifadhi makumi ya maelfu ya wakimbizi katika kambi.
    Taarifa ya serikali imesema kuwa uwepo wao katika himaya yake,ikiwa ni karibu na taifa lao,ni hatari kwa wahusika wote.

    Wiki iliopita wataalam wa Umoja wa Mataifa waliliambia baraza la usalama la umoja wa mataifa kwamba Rwanda imewasajili na kuwapa mafunzo wakimbizi kutoka Burundi wakiwemo watoto ambao walitaka kumuondoa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza kutoka madarakani.

    Burundi kwa mara kadhaa imeilaumu Rwanda kwa kuwaunga mkono waasi walio na lengo la kuipindua serikali ya Bujumbura.
    Hatahivyo Kigali imekana madai hayo.

    Rais Pierre Nkurunziza
    ''Rwanda imechukua jukumu la kuwalinda na kuwaangalia wakimbizi'',ilisema taarifa ya serikali.
    Hatahivyo imebainika katika eneo la maziwa makuu kwamba uwepo wao kwa kipindi cha mda mrefu karibu na taifa lao ni hatari kwa wahusika wote.

    Taifa la Burundi limekuwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe tangu Nkurunziza kutangaza mipango mwezi Aprili kuwania muhula wa tatu,ambao alishinda.Mamia ya raia wameuawa na wengine 230,000 kulitoroka taifa hilo.

    Maandamano ya Burundi
    Rwanda inawahifadhi zaidi ya wakimbizi 70,000 ikiwemo 24,000 wanaoitwa wakimbizi wa mijini.Kambi kubwa ya wakimbizi nchini humo ni ile ya Mahama.

    Hakuna kambi nyengine zozote za wakimbizi zinazojulikana isipokuwa kambi ndogo za muda kwa wale wanaongojea kupelekwa katika kambi ya Mahama.

    Chanzo; BBC

  • Watu 21 Watiwa Mbaroni kwa Mauaji ya Kondoo Na Mbuzi Mvomero, Morogoro

     Wenyeviti wa Serikali za vijiji vya Mkindo, Patrick Longomeza (52) na mwenzake wa Dihombo, Christian Thomas (50) pamoja na wananchi wengine 19 wanashikiliwa na Polisi kwa tuhuma za kujeruhi mifugo mali ya mwanamke mfugaji wa Kimasai, Katepoi Nuru (36) wa Kijiji cha Kambala wilayani Mvomero Mkoa wa Morogoro.

    Mbali na wenyeviti wa vijiji hivyo, pia Polisi wamemtia mbaroni kinara wa uhamasishaji vijana wa kimasai kuwapiga na kuwajeruhi wakulima wanaolima katika Bonde la Mgongola, Kashu Moreto (68) kwa tuhuma za kulisha mazao na kumjeruhi mguu wa kulia, mkulima Ramadhan Juma (19), mkazi wa Dihombo.

    Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Morogoro, Leonard Paulo alisema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la awali lililotokea Februari 7, mwaka huu mchana katika Kijiji cha Kambala.

    Alisema kabla ya kukatwa kwa mifugo ya mwanamke huyo, kundi la ng’ombe zaidi ya 50 likiwa na wachungaji zaidi ya watatu wa Kimasai walilisha shamba la mpunga ekari moja la mkulima Rajab Issa (31) aliyewazuia na ghafla walijitokeza vijana wanaosadikiwa kuwa ni Morani wa kimasai na kuwachukua ng’ombe hao kwa nguvu.

    Aliwataja wengine waliotiwa mbaroni mbali na wenyeviti hao ni Issa Ally (66), Hussein Said (25), Juhudi Amimu (25), Emily Pascal (40) na Mkude Milikioni (25) ambao wote ni wakazi wa Kijiji cha Mkindo.

    Wengine waliokamatwa ni Ally Bakari (25), Gerald Mbegu (22), Miraji Noras (22), Mengi Mbegu (32), Kudura Abdi (35), na wanawake wawili Angelina Sadiki (20), Hadija Msanga (30), wote wakazi wa Kijiji cha Mkindo.

    Pia wamo Mustafa Malugo (35), Charles Moris (40), Amset Alfred (42), Hassan Mohamed (46) pamoja na Hapifan Paulo ambao wote hao ni kutoka katika Kijiji cha Dihombo wilayani Mvomero.

    Kamanda Paulo alisema baada ya vijana hao wa kimasai kuingia kulisha katika shamba la Issa, alijaribu kuwazuia, lakini ghalfa walijitokeza vijana wanaosadikiwa kuwa ni morani wa kimasai na kuwachukua ng’ombe hao kwa nguvu, na mkulima huyo alitoa taarifa katika Kituo cha Polisi Mvomero.

    Lakini alisema Februari 8, mwaka huu mchana wakati tukio hilo likishughulikiwa, kikundi cha watu kilivamia nyumbani kwa Nuru Kipande (76) na kumkuta kumkuta Ketepoi Nuru (36) akiwa nyumbani huku mifugo aina ya mbuzi, kondoo na ndama wakiwa malishoni.

    Kwa mujibu wa Kamanda, kundi hilo lilinyang’anya mifugo hiyo na kisha kumnyang’anya mwanamke huyo simu yake ya mkononi ili asiombe msaada na kisha kuipeleka mifugo hiyo porini na kuanza kuikatakata kwa vitu vyenye ncha kali .

    Kamanda alisema watuhumiwa waliokamatwa wanaendelea kuhojiwa na wengine kutafutwa na wote waliohusika katika tukio hilo watafikishwa mahakamani, na kutoa onyo kwa watu wote kuacha kujichukulia sheria mkononi.
  • PICHA: Majangili 9 Wanaotuhumiwa Kutungua Helkopta Wafikishwa Mahakamani

    Watu tisa wamefikishwa mahakamani wakituhumiwa kutungua helikopta iliyokuwa ikifanya doria kwenye Pori la Akiba la Maswa wilayani Meatu, Simiyu na na kumuua rubani wake.

    Mbali na kutungua chopa na kumuua rubani wake, Rogers Gower, raia wa Uingereza, watu hao pia wameshtakiwa kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuuza na kumiliki silaha kinyume cha sheria.

    Washtakiwa hao walifikishwa mbele ya Mahakama ya Mkoa wa Simiyu jana wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, huku umati wa wananchi wakifurika na kusababisha hekaheka mahakamani hapo.

    Yamiko Mlekano, ambaye ni wakili mwandamizi wa Serikali, alidai kuwa washtakiwa wote kwa pamoja wanakabiliwa na kesi tatu; uhujumu uchumi, mauaji na umiliki wa silaha bila ya kibali.

    Katika kesi namba mbili ya mauaji, Wakili Yamiko alidai kuwa Shija Mjika (38), Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42) na Moses Mandagu walitungua helikopta hiyo Januari 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba iliyoko Kijiji cha Makao wilayani Meatu na kumuua rubani Gower.

    Mlekano alidai kuwa katika kesi ya uhujumu, mshtakiwa namba moja Iddy Mashaka (49) anadaiwa kujihusisha na kuratibu tukio la uhujumu uchumi kinyume na sheria.

    Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi Mwandamizi, John Nkwabi, wakili huyo alida kuwa mshtakiwa alitenda kosa hilo Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu kwa kumshauri mshtakiwa namba mbili, Shija Mjika (38) kuua wanyama wasioruhusiwa.

    Katika shtaka la pili, watu saba; Njile Gunga (28), Dotto Pangali (42), Moses Mandagu (48), Dotto Huya (45), Mwigulu Kanga (40), Mapolu Njige (50) na Mange Barumu (47) pia wanashtakiwa kwa kuhujumu uchumi.

    Aliieleza mahakama kuwa kati ya Januari 21 na 29 katika wilayani Meatu, washtakiwa walipanga na kuratibu tukio la kuwinda wanyama aina ya tembo bila ya kibali cha Serikali.

    Wakili Mlekano alidai kuwa shtaka la tatu la uwindaji wanyama wasioruhusiwa linawakabili mshtakiwa wa pili hadi tisa na wanadaiwa kutenda Januari 26 na 29 kwenye Hifadhi ya Mwiba Kijiji cha Makao wilayani Meatu wa kumuua tembo mwenye thamani ya Sh32,891,100 bila ya kibali.

    Katika shtaka la nne, mshtakiwa namba mbili na tisa wanatuhumiwa kumiliki nyara za Serikali kinyume na sheria.

    Washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo Januari 29 na Februari Mosi wilayani Meatu ambako walikamatwa na meno ya tembo yenye uzito wa kilo 31 na thamani ya Sh32,891,100.

    Katika shtaka namba tano, Mashaka na Mjika wanashtakiwa kwa kuuzaji nyara za Serikali kinyume na sheria na kwamba walitenda kosa hilo kati ya Januari 6 na Februari Mosi wilayani Meatu.

    Hakimu Nkwabi alisema washtakiwa hawatakiwi kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na uwezo wa kusikiliza kesi hiyo na aliahirisha hadi Februari 24 zitakapotajwa tena.

    Katika kesi ya tatu ambayo ni kukutwa na silaha kinyume cha sheria iliyosomwa mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya, Mary Mrio, washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka matano.

    Washtakiwa hao ni Buluma, Mjika, Pangani, Ngunga, Mandagu, Huya na Kanga ambao baadhi yao walikiri kumiliki silaha na risasi kinyume cha sheria akiwamo Njile anayedaiwa kutungua helikopta hiyo.

    Washtakiwa hao walikiri mashtaka mawili ambayo ni kukutwa na bunduki aina ya Riffle 303, wakati Ngunga na Mandagu walikiri shtaka la tatu, nne na tano la kukutwa na silaha na risasi bila ya kibali.

    Hata hivyo, Hakimu Mrio alishindwa kutoa hukumu kwa washtakiwa waliokiri kosa kutokana na kutokuwapo kwa vielelezo mahakamani hapo, hivyo kesi hiyo iliahirishwa hadi leo. 
    Watuhumiwa wakiwa ndani ya gari la polisi, baada ya kufikishwa kituo cha polisi Bariadi wakitokea wilayani Meatu kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.
    Njile Gunga (28) Huyu ndiye Jangili anadaiwa kutungua helkopta katika pori la Akiba la Maswa lililopo katika Wilaya ya Meatu Mkoani, ambapo katika tukio hilo rubani wa helkopta hiyo Rodgers Gower (37) raia wa uingereza huku Mwenzake Nicholas Beste (43) raia wa Afrika Kusini akinususrika kifo.
    Iddy Mashaka (49) ambaye ndiye alikuwa Mkuu wa kitengo cha Interejensia katika hifadhi ya taifa Ngorongoro, ambaye anadaiwa kuwa kiunganishi Mkuu wa kutekeleza tukio la kutunguliwa kwa helkpta hiyo.
    Hali ya ulinzi na usalama ilivyokuwa imehimarsihwa mahakamani pamoja na kituo cha polisi Bariadi leo hii.
    Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Elaston Mbwilo akionyeshwa watuhumiwa wa ujangili ambao walihusika kutungua Helkopta.
    Watuhumiwa wakiwa Mahakamani.
    Wakazi wa Mji wa Bariadi wakiwa wamefurika  katika viwanja vya Mahakama ya wilaya hiyo kushuhudia watuhumiwa hao.
    Chanzo; Mpekuzi
  • Watanzania Wapelekwa Uganda Kupiga Kura

    Mgombea wa urais katika uchaguzi ujao nchini Uganda, Amama Mbabazi amedaia kuwa kundi la raia wa kigeni wamekuwa wakisafirishwa hadi nchini humo kwa ajili ya kumpigia kura Rais Yoweri Museveni.

    Mbabazi ambaye ni mgombea huru alisema, mamia ya raia kutoka nchi za Tanzania na Rwanda wamekuwa wakiwasili nchini humo ili kukisaidia chama tawala na mgombea wake kushinda kwenye uchaguzi huo.

    Mwanasiasa huyo ambaye kabla hapo alikuwa waziri mkuu chini ya utawala wa Rais Museveni, alitahadharisha wananchi kuwa macho na mwenendo huo, huku akiwataka kuchukua hatua kuzuia aina yoyote ya udanganyifu.

    Waziri Mkuu huyo wa zamani ambaye alikuwa akizungumza na waandishi wa habari alisema yeye binafsi pamoja na timu yake ya kampeni itaendelea kuwa macho kufuatilia mwenendo huo.

    “Watu wana njia nyingi za kufanya udanganyifu. Idadi kubwa ya Watanzania wamekuwa wakiwasili nchini kwa ajili ya kupiga kura. Pia, tumeshuhudia watu wakitoka Rwanda na kupiga kura.

    "Tumebaini njama zao na sisi wananchi lazima tuwe macho kuwabaini watu hao siku ya kupiga kura itapowadia,” alisema Mbabazi. Uchaguzi Mkuu nchini humo utafanyika Februari 18.
  • Watu zaidi ya 56 wafariki Nigeria

    Maafisa wa magharibi mwa Nigeria wanasema watu zaidi ya hamsini wameuwawa katika shambulio lililotokea katika kambi ya watu waliokimbia makazi yao katika jimbo la Borno.

    Wanawake wawili walirusha bomu ,na watatu alikamatwa na polisi,hukuakikana kuhusika katika shambulio hilo kwa kudai kuwa wazazi wake wako kwenye kambi hiyo hivyo haiwezekani kwa yeye kufanya kitendo hicho

    Zaidi ya watu milioni mbili wamelazimika kuyakimbia makaazi yao kutokana na mashambulio ya kushtukiza katika kipindi cha miaka sita iliyopita kulikosababisha na kundi la wanamgambo wa Boko Haram.

    Chanzo; BBC
  • Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Yaunda Kanuni Zitakazowaongoza Wabunge Wake

     Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni (KUB) imeunda kanuni zitakazowaongoza wabunge wake kuendesha shughuli mbalimbali za chombo hicho cha uwakilishi.

    Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema, Salum Mwalimu aliwaambia wanahabari jana kuwa kanuni hizo ambazo zimeundwa kwa kushirikisha vyama vyote vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) zitasaidia kuondoa holela iliyokuwa ikijitokeza awali ndani ya KUB.

    Mwalimu, ambaye chama chake ndiyo kinaongoza kambi hiyo, alisema Chadema inaipongeza hatua hiyo kwa kuwa imeonyesha kuzaa matunda katika mkutano wa pili wa Bunge la 11 uliomalizika wiki iliyopita.

    Kanuni hizo za kambi rasmi ya upinzani, kwa mujibu wa Mwalimu zimeanzishwa kwa kufuata kanuni ya 16, ibara ya 4 ya Kanuni za Kudumu za Bunge ambayo inasema:

    “Vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni vinaweza kutunga kanuni za vyama vya kwa ajili ya uendeshaji bora wa shughuli za vyama hivyo bungeni.”

    Mwalimu alisema kanuni hizo tayari zimeshasaidia uteuzi wa wawakilishi katika vyombo vya kimataifa kupitia Bunge.

    Alisema katika utaratibu wa kanuni hizo mpya jambo likishaamriwa kwenye vikao vya umoja huo hakuna mtu wa kupinga na ikitokea mbunge husika akazivunja hatua za kinidhamu zitachukuliwa.

    “Kwa sasa hamna tena songombingo ya kupata nafasi za uwakilishi ndani ya Bunge. Likipita jambo ndani ya caucus (kikao cha chama) basi limepita...hakuna tena kuvujisha siri ndiyo maana safari hii hata waandishi ilikuwa vigumu kupata taarifa za ndani,” alisema.

     Akizungumzia umeya Dar es Salaam alisema kuna hila za wazi za kutaka kuongeza wajumbe wasiotakiwa katika uchaguzi hasa kutoka Ilala na Kinondoni.
  • Maelfu wauawa kinyama Syria

    Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema maelfu ya raia wa Syria waliowekwa kizuizini wamekuwa wakifa kinyama kwa maelfu kwa kiwango kinachofikia uhalifu dhidi ya binadamu.

    Maafisa wa Umoja wa mataifa waliofanya uchunguzi huo wanasema raia wa Syria ambao wamekuwa wakiunga mkono waasi au kuipinga serikali wamekuwa wakikamatwa hapo hapo.

    Wakati huo huo Wakati Majeshi Syria yakiendelea na mapambano katika mji wa Allepo, Uturuki imesema kipaumbele chake cha kwanza ni kuwapa misaada wale waliokimbia makazi yao kutokana na vita.

    Naibu Waziri Mkuu Numan Kurtulmus amesema raia wa Syria wapatao elfu sabini na saba wanapatiwa msaada na Uturuki katika kambi katika eneo la mpakani.

    Imepangwa katika siku za usoni katika maeneo yaliyoathirika kwenye eneo hili, idadi kubwa ya wakimbizi wapatao laki sita, wanaweza kukusanyika katika eneo la mpaka wa Uturuki na Syria. kama leo karibu watu elfu sabini na saba wamepatiwa makazi kwenye kambi zilizojengwa mpakani mwa Uturuki na shirika lisilo la kiserikali la AFAD. kama unavyojua tumewachukua waarabu elfu tano na wasirya wenye asili ya Uturuki nchini Uturuki wiki iliyopita."

    Naye Waziri wa mpito wa Syria Hussein Bakri ameelezea kusikitishwa na kutokana na hali ilivyo"Haya ni mashambulizi ya mabomu yasiyo ya kawaida. Yamesababisha watu zaidi ya sabini elfu kukimbia makazi yao katika mji wa Alleppo kwa ujumla, na hasa eneo la kaskazini.Kama hali itaendelea kama hivi sasa, itasababisha watu zaidi laki nne kutoka Jimbo la Allepo na mji wa Allepo pekee kukimbia makazi yao. Ni wazi kabisa Urusi imedhamiria kuuzunguka na mji wa Allepo, kama ilivyotokea katika maeneo mengine ya Syria..

    Chanzo; BBC
  • Wingu Zito Laendelea Kutawala Ufisadi Wa Mabilioni NIDA,Yadaiwa Kitambulisho Kimoja Kimegharimu Sh 89,800


    Wingu  zito limetanda ndani ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kuhusu matumizi ya  Sh bilioni 179.6 ambako kila kitambulisho  cha taifa kimegharimu Sh 89,800 zikiwamo gharama za utawala

    Hayo yamebainika  siku chache baada ya Rais Dk. John Magufuli kushangazwa na watendaji wa mamlaka hiyo ikizingatiwa vitambulisho vilivyokwisha kutengenezwa hadi sasa havifiki   milioni mbili na havina saini.

    “Utaona ugumu wa kuongoza, nchi inatawaliwa na madudu ya kila aina.  Wapo watu wanacheza na fedha wanavyotaka wakati wapo watu masikini sana  wengine wanataka bodi zao wakakae Ulaya.

    “Hapo ndipo tulipofikia, wengine wanalipwa mshahara wa Sh milioni 35 kwa mwezi…naomba mniombee kabla ya kunihukumu, toeni hukumu kwa haki kwa hawa wanaotaka kuifikisha nchi pabaya, toeni hukumu zao haraka,” alisema.

    Rais Dk. Magufuli, licha ya kushangazwa na hali hiyo, alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilipewa Sh bilioni 70 lakini iliweza kutengeneza vitambulisho   23,253,982 ambavyo vilikuwa na saini ya kila mpiga kura na kila kimoja kimegharimu Sh 3,010.

    Kutokana na hali hiyo, tofauti ya gharama kati ya kitambulisho kimoja cha NIDA na cha NEC ni Sh 86,790.

    Pamoja na hayo, hivi sasa Watanzania wanasuburi   ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Juma Assad, kuhusu  matumizi ya fedha hizo za NIDA.

    Januari 26 mwaka huu, Rais Magufuli alitangaza kumsimamisha kazi ili kupisha uchunguzi dhidi yake, Mkurugenzi Mkuu wa NIDA, Dickson Maimu.

    Maimu alisimamishwa kazi pamoja na maofisa wengine wanne, kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za Serikali.

    Maofisa hao ni Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Joseph Makani, Ofisa Ugavi Mkuu, Rahel Mapande, Mkurugenzi wa Sheria, Sabrina Nyoni na Ofisa Usafirishaji, George Ntalima.

    Akitangaza uamuzi huo, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Sefue, alisema taarifa zilizomfikia Rais zinaonyesha kuwa NIDA hadi wakati huo ilikuwa imetumia Sh bilioni 179.6, kiasi ambacho ni kikubwa.

    Alisema Rais angependa ufanyike uchunguzi na ukaguzi kujua jinsi fedha hizo zilivyotumika, maana amekuwa akipokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na kasi ndogo ya utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.

    Licha ya kumuelekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, afanye ukaguzi maalumu wa hesabu za NIDA  ukiwamo ukaguzi wa “value for money” baada ya kuthibitisha idadi halisi ya vitambulisho vilivyotolewa hadi sasa, pia aliitaka Takukuru ifanye uchunguzi kujiridhisha kama kulikuwa na vitendo vya rushwa au la.

    Credit: Mtanzania
  • Jaji Damian Lubuva Amtaka ' Lowassa' Aache Kuupotosha Umma

     Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec), Jaji Damian Lubuva amewataka wanasiasa walioshindwa kwenye Uchaguzi Mkuu waache kujitangaza kuwa walishinda, akisema wanapotosha wananchi.

    Kauli hiyo ya Jaji Lubuva imekuja siku chache baada ya aliyekuwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa kudai kuwa kama si matokeo kuchakachuliwa, alikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa sababu wananchi walishaichoka CCM na wakawa wanataka mabadiliko.

    Lowassa alisema hayo katika mahojiano maalum na waandishi wa habari ofisini kwake, akisema yeye na Ukawa walishinda kwa kishindo isipokuwa matokeo yalivurugwa makusudi ili CCM iendelee kubaki madarakani.

    Jana, akiwa kwenye mkutano wa tathmini kati ya NEC na asasi za kiraia kuhusu utoaji elimu kwa mpigakura uliofanyika Dodoma, Jaji Lubuva alisema uchaguzi umeshapita na kilichobaki sasa ni kufanya kazi tu.

    Bila ya kutaja jina la mwanasiasa huyo, Jaji Lubuva alisema kama kuna mtu alishindwa katika uchaguzi uliopita, ajipange kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao mwaka 2020.

    “Hata wananchi wanawashangaa kwa kuwa wao ndio walioamua ni nani anafaa kuwaongoza,” alisema Jaji Lubuva.

    Alisema kuwa NEC ilikuwa inapokea matokeo ya uchaguzi kutoka majimboni na kuyasoma kama yalivyotumwa na katika hilo hakuna wakala hata mmoja wa chama ambaye aliyapinga matokeo hayo.

    “Sasa nashangaa kuna baadhi ya wagombea wanaotaka Tume ifukuzwe kazi eti tu kwa sababu wao hawakushinda. Naomba ifahamike kwamba katika kila uchaguzi duniani kuna kushinda na kushindwa.

    "Sasa kama kila atakayeshindwa atataka tume ifukuzwe kazi hapatakuwa na tume ya uchaguzi kwa sababu kila atakayekuwa anashindwa atakuwa anataka tume ifukuzwe kazi,” alisema Jaji Lubuva.

    Chadema, ambayo iliungana na vyama vitatu kuunda Ukawa, iliitaka NEC kusitisha utangazaji matokeo ikidai kuwa kilichokuwa kikitangazwa ni tofauti na takwimu walizokusanya kutoka majimboni. Lakini NEC ikaendelea kutangaza.

    Baadaye, Chadema ililalamika ikidai kituo chao cha kukusanya na kujumlisha matokeo kilivamiwa na polisi na kompyuta kuchukuliwa na hivyo kuvuruga ufuatiliaji wao wa matokeo.

    Kwa upande wake mkurugenzi wa huduma kutoka NEC, Emmanuel Kavishe alisema kuwa Tume inafanya kazi kwa mujibu wa sheria na Katiba na kwamba hata siku moja haijawahi kumpendelea au kumuonea mtu yeyote.

    Katika uchaguzi wa urais, John Magufuli alipata kura milioni 8.8 huku Lowassa akipata milioni 6.07.
  • Mwaka mpya wa nyani washerehekewa China

    Mamilioni ya watu wenye asili ya China, duniani kote wanasheherekea mwaka mpya wa ki China .

    Baruti nyingi zilirushwa angani mjini Beijing ikiwa ni ishara ya kusheherekea siku ya kwanza ya mwaka mpya wa nyani,Nyani wakiwa ni miongoni mwa wanyama kumi na mbili wanaotumiwa kati ya alama za kichina katika masuala ya utabiri.

    Nako mjini Yokohama nchini Japan, wao wanasheherekea siku kuu hii kwa kuhesabu muda huku wakicheza ngoma ya asili ya kucheza na simba.

    Maadhimisho ya sherehe hizi za mwaka mpya zinajumuisha watu kula pamoja,kufanya usafi na familia kuwa pamoja huku wakirusha fashi fashi angani.
  • Polisi Watatu Wafa kwa Ajalii Msafara wa Rais Magufuli

    Askari polisi watatu wamefariki dunia na wengine wawili wamejeruhiwa baada ya gari lao lililokuwa kwenye msafara wa Rais John Magufuli kutoka Singida kwenda Dodoma, kupasuka tairi na kupinduka.
    Rais Magufuli alikuwa mjini Singida alikokuwa amekwenda kushiriki maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM.

    Hiyo ni mara ya pili kwa askari kufariki wakiwa kwenye msafara wa Dk Magufuli baada ya aliyekuwa akiongoza msafara wake wakati wa kampeni kugongana na dereva bodaboda katika eneo la Ubungo jijini Dar es Salaam.

    Askari huyo alikuwa kwenye pikipiki maalumu iliyokuwa ikiongoza msafara wakati Dk Magufuli akitoka katika Hospitali ya Lugalo kuaga mwili wa aliyekuwa mbunge wa Ludewa, Deo Filikunjombe.

    Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, ACP Thobias Sedoyeka alisema ajali hiyo ilitokea saa 9.40 alasiri, katika Kijiji cha Isuna, Wilaya ya Ikungi mkoani humo baada ya moja ya matairi ya gari hilo kupasuka na dereva kushindwa kulimudu.

    Aliwataja waliofariki kuwa ni Mkaguzi Mwajelo, Sajenti Elias Mrope na Sajenti Gerard.

    Waliojeruhiwa ni Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoani Singida (RCO), Peter Majira (50
    na PC Charles Simon (34) ambao wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Manyoni.

    Gari hilo lililopata ajali ni lile lililokuwa limetangulia ili kufagia barabara kabla ya msafara wa Rais, likiongozwa na Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani cha mkoa huo.

    Sedoyeka alisema miili ya askari hao imehifadhiwa katika chumba cha maiti cha hospitali ya mkoa huo.

    Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Manyoni, Kitundu Jacks alisema hali za majeruhi waliofikishwa kwenye hospitali hiyo zinaendelea vizuri.

    “Mrope ndiye aliyeletwa akiwa kwenye hali mbaya, alikuwa amevunjika mbavu na mkono na akafa mara tu baada ya kufikishwa hospitalini hapa. Majeruhi wengine wamepata michubuko na wanaendelea vizuri,” alisema. 
  • Tetemeko baya lakumba Taiwan

    Tetemeko kubwa la ardhi limekumba Taiwan Kusini, na kuangusha jengo moja la ghorofa 17 ambapo hadi kufikia sasa watu watatu wamethibitishwa kufariki.

    Tetemeko hilo la kipimo cha Ritcher 6.4 lilitokea karibu na mji wa Tainan.

    Zaidi ya watu 200 wameokolewa kutoka kwa jengo hilo, ingawa waokoaji wangali wanajaribu kuwafikia watu wengine ambao inadhaniwa wangali wamekwama katika mabaki ya jengo hilo.

    Tetemeko hilo liligonga usiku wa manane wakati watu wengi walikuwa wamelala.

    Kumetokea matetemeko mengine madogo matano mda mfupi baada ya tetemeko hilo kuu.

    Idara ya kusimamia maswala ya chini ya radhi inasema kuwa tetemeko hilo lilitokea sehemu ya juu pekee, hali ambayo husababisha madhara makubwa zaidi.


    Chanzo: BBC
  • GET A FREE QUOTE NOW

    Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit, sed diam nonummy nibh euismod tincidunt ut laoreet dolore magna aliquam erat volutpat.