![]() |
Maiti |
Familia moja nchini Canada iliishi
na maiti katika chumba cha juu cha nyumba yao kwa miezi sita kwa kuwa
waliamini marehemu atafufuka iwapo wataendelea kumuomba mungu,lakini
mwili huo ukapatikana baada ya familia hiyo kushindwa kulipa mkopo
waliochukua kununua nyumba hiyo.
Peter Wald mwenye umri wa miaka 52 alifariki mnamo mwezi machi mwaka 2013 kwa kile mamlaka inasema ni sababu za kawaida kufuatia maambukizi ya mguu wake yanayodaiwa kusababishwa na ugonjwa wa sukari.
Mkewe Kaling Wald alimwacha kitandani na kufunga chumba hicho katika nyumba yao ya Hamilton ,Ontario ili kuzuia harufu kali iliokuwa ikitoka chumbani humo kuwafikia watu waliokuwa wakiishi nyumbani humo.
Kama vile Yesu alivyomfufua Lazaro baada ya siku ya nne ,pia yeye aliamini kwamba Mungu atamfufua mumewe wakili wa mwanamke huyo alisema.
0 comments:
Post a Comment