![]() |
Rais Abdel Fattah el-Sisi wa Misri akiwafariji wakuu wa Kanisa la Coptic |
Rais wa misri Abdel Fatah Al-Sisi ameutaka umoja wa mataifa kuidhinisha hatua za kijeshi za kimataifa dhidi ya kundi la Islamic State nchini Libya.
Akizunguma na kituo kimoja cha radio cha Ufaransa ( Europe One) rais Sisi alisema kuwa watu nchini Libya wanataka hatua kali kuchukuliwa ili kuleta usalama na udhabiti nchini mwao.
Al sisi alisema ''Hatutawaruhusu watoto wetu wachinjwe ovyo na hawa magaidi.''
Wito wa rais Sisi unakuja siku moja baada ya ndege za kivita za Misri kushambulia ngome za Islamic State kulipiza kisasi kuuawa kwa wamisri wa dhehebu la Coptic nchini Libya siku ya Jumamosi.
Hapo jana , Taarifa kutoka Misri zilisema kuwa, ndege za kijeshi ziliwashambulia wapiganaji wa jihadi nchini Libya kwa mabomu, baada ya kutolewa kwa mkanda wa video ulioonyesha wakristo wa Misri wa madhehebu ya Coptic
0 comments:
Post a Comment