• Umeisikia hii bukta yenye thamani ya milioni 80?


    Bukta ya Amir Khan ambayo ataivaa jumamosi hii kwneye pambano lake dhidi ya Devon Alexander .
    Siku zote ubunifu umeonekana kuwa kitu muhimu kwenye mambo mablimbali hususan michezo ambako watu huwekeza fedha nyingi sana kwenye kutengeneza taswira za wanamichezo ambazo huuzika kama bidhaa .

    Bondia Muingereza Amir Khan ametoa mpya baada ya kutangaza kuwa atavaa bukta yenye dhahabu halisi katika pambano lake linalofuata ambalo atapambana na Mmarekani Devon Alexander .
    Bukta ya Amir Khan ambayo ataivaa jumamosi hii kwneye pambano lake dhidi ya Devon Alexander .


    Thamani ya ukanda wa dhahabu ambao utakuwa umeinakshi bukta ya bondia huyo mwenye asili ya Pakistan ni paundi 30,000 ambayo ukithaminisha kwa fedha ya Tanzania ni sawa na shilingi milioni themanini (81,836,512.34) .

    Baada ya kuvaa bukta hiyo Amir Khan anatarajiwa kuipiga mnada ambapo itauzwa kwa fedha nyingi sana .


    Khan atapanda ulingoni jumamosi hii katika pambano hilo la kuwania ubingwa wa Uzito wa Welter unaotambuliwa na WBC kupambana na Devon Alexander na endapo atashinda huenda kaapata nafasi ya kupambana na Floyd Mayweather .
  • 0 comments:

    Post a Comment

    GET A FREE QUOTE NOW

    Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit, sed diam nonummy nibh euismod tincidunt ut laoreet dolore magna aliquam erat volutpat.