Mgombea Ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA katika Jimbo la Arusha,GODBLEES LEMA ameibuka mshindi na kutangazwa kuwa mbunge mteule wa jimbo hilo.
Katika uchaguzi huo ulioshirikisha vyama vitano vya siasa, LEMA amepata kura Elfu-68 na 848 kati ya kura Laki-1,Elfu-4 na 353 zilizopigwa akifuatiwa na mgombea wa Chama cha Mapinduzi,PHILEMON MOLLEL aliyepata kura Elfu-35 na 907.