![]() |
Maandamano Garissa |
Waandamanaji pia wameelezea kutoridhika na vyombo vya usalama nchini humo wakisema havikuchukua hatua za kutosha kutoa ulinzi kwa waliouawa na kwa raia wengine kwa jumla.
Wazazi, jamaa na marafiki wa wanafunzi waliouawa katika chuo kikuu cha Garissa wamekuwa wakiendelea kuwasili katika eneo hilo kuitambua miili ya wapendwa wao.
Waliojeruhiwa wanaendelea kupata matibabu .

Wakati huo huo rais wa Somalia, Hassan Sheikh Mohamoud, amesema Somalia na Kenya zinafaa kuimarisha uhusiano wao katika mapambano dhidi ya ugaidi.
Tamko hilo linajiri siku moja baada ya shambulio hilo la Alshaabab katika chuo kimoja kikuu mjini Garrisa.
Chanzo; BBC
0 comments:
Post a Comment