Rooney anauguza jeraha la kifundo cha mguu.
Fowadi huyo mwenye umri wa miaka 30 hakuweza kumaliza mechi waliyotoka sare 1-1 ugenini Leicester City wikendi iliyopita na atahitajika kusubiri muda zaidi kuchezea klabu hiyo mechi yake ya 500.
Meneja Louis van Gaal amesema tatizo hilo ni mbaya zaidi ya ilibyodhaniwa.
Ratiba ya mechi za EPL wikendi
United wanahitajika kushinda mechi ya ugenini dhidi ya Wolfsburg Jumanne kujihakikishia nafasi hatua ya muondoano.
Difenda wa United Marcos Rojo naye ameumia kwenye bega.
Phil Jones na Ander Herrera kwa upande mwingine hawataweza kuchezea klabu hiyo dhidi ya West Ham, ingawa Jesse Lingard atarejea.